LABDA Media zinamjengea Presha Binti Coco Gauff , akiwa na umri wa miaka 15 tayari anapewa " Hype" .
haikua shida kwa Mrusi Anastasia Potapova kutinga raundi ya pili mbele ya Mmarekani Coco Gauff.
- Venus Williams atamvaa mukraine Elina Svitolina , wakati Mwanadada Catheline McNailly atavaa kigingi dhidi ya Serena Williams kunako raundi ya Pili.
- Bingwa wa michuano ya Wimbledon Simona Halep hapo jana aliibuka na ushindi wa kwanza wa US Open toka mwaka 2016 . Kwamba tangu mwaka 2016 hakuwai vuka raundi ya kwanza .
- Bianca Vannesa yeye alikua na siku safi mbele ya binti Volynets baada ya ushindi wa " Straight set " 6-2, 6-4.
- Naomi Osaka ameanza kwa tabu dhidi Anna Blinkova , akisonga mbele katika seti ya Mwisho (6-4,6-7(5),6-2 .
Taifa la Belarus walishuhudia Aryna Sabarenka akimchapa Vick Azarenka na Aryna kusonga mbele kunako US Open .
No comments:
Post a Comment